KAF FARMS
1. Wasifu Mfupi Wa Shamba
KAF Farms inajishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula, mifugo, na misitu. 2. Muhtasari wa Shamba darasa
KILIMA AGROPIARY FARMS/KAF FARMS
KAF FRMS ina ekari zisizo pungua 100.
KAF itatumia jukwaa la wataalamu wetu na washirika kwa kutoa huduma mbalimbali zinazohusiana na kilimo, ufugaji mf. SHAMBA DARASA pamoja na kusaka masoko ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. 3. Maono na Malengo ya MkulimaMaono:
Malengo:1. MALENGO YA MUDA MREFUKufanya mradi wa KAF Farms kufikia mikoa mingi zaidi Tanzania bara na visiwani. Kuifanya KAF farms kuwa wenye mfumo bora ambao unaweza kutumika hata katika Franchising. 2. MALENGO YA MUDA MFUPI Kurasimisha mashamba yetu yaliyopo Bagamoyo, Kiwangwa na Tabora. Kuongeza kilimo kwenye mazao yenye tija pamoja na kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki kwa kuongeza mizinga. Kuongeza wataalamu wa nyanja tofauti tofauti katika mradi huu ili kuongeza ufanisi na weledi. 4. Manufaa kwa Jamii Inayozunguka Mradii. Ushirikiano wa Jamii:KAF FARMS Imeajiri vijana wasiopungua 10 mashambani. Maatarajio yetu ni kuwafikia wananchi wa karibu ya shamba 100 watafaidika na mradi huu ndani ya kipindi cha mwaka 1. ii. Wakulima waliofunzwa:Zaidi ya watu 30 wamefaidika na KAF FARMS na tunategemea wakulima wengi zaidi watakuja kujifunza kuhusu kilimo biashara. iii. Kazi Nyinginezo Katika Shamba Hili Pia KAF Farms ina mpango wa kuanzisha kilimo cha uyoga na uzalishaji wa mbolea itokanayo na takataka za mfumo wa uzalishaji wa uyoga pamoja na mazao mengine shambani kama vile masalia ya mimea na takataka za mifugo. Pia KAF farms inatarajia kuanzisha mradi wa nishati safi itokanayo na kinyesi cha mifugo na mabaki ya mbogamboga (BioGas) ambayo kwa kuanza itatumika kama nishati katika kuzalisha mafuta ya chikichi na matumizi mengine yanayohitaji nishati hapo shambani. 5. Mafanikio Ya KAF FARMS:KAF Farms - Makurunge ni shamba lenye ekari 40 za mraba. Mradi huu una miaka 6 Tumefanikiwa kuotesha zao la michikichi ipatayo 300 mizinga ya nyuki 70 miembe 2000, mikorosho ekari 3, mikaratusi, migomba, maembe ekari 3, minazi, mastafeli pamoja na fenesi. 6. Jinsi KAF FARMS Inavyochangamkia Fursa Za Utalii wa Kilimo, Mila, Utamaduni na Asili
|
Wito Kwa Jamii (CALL TO ACTION)
KAF FARMS ipo chini ya usimamizi wa mradi wa SHAMBA DARASA. Jamii inapaswa kutembelea shamba hili kujifunza kwa vitendo juu ya mbinu bora za kilimo biashara kwa mazao kama vile Una wazo la kufanya kazi au Kushiriana na KAF FARMS? KAF FARMS inawakaribisha wanaohitaji kazi mashambani, wanunuzi wa mazao na wawekezaji.
ZAIDI KUHUSU KAF FARMS:
|